Jarida la Darubini ya Kiswahili (JADAKI)  ni jarida la kimataifa  linaloratibiwa na Idara ya Lugha na Stadi za Mawasiliano katika Kitivo cha Sayansi za Jamii, Chuo Kikuu Mzumbe. Hili ni Jarida linalotumia lugha ya Kiswahili, na linachapisha makala kwa mwaka mara moja katika nyuga zote za Kiswahili na utamaduni wa Mswahili. Hivyo, tunawakaribisha wadau wote kuchangia maarifa kupitia nyuga zilizobainishwa ili kuendelea kukuza, kupanua, na kuipa heshima lugha yetu ya Kiswahili ambayo ni utambulisho wetu.